Quantcast
Channel: BUKOBA WADAU
Viewing all articles
Browse latest Browse all 4177

UFUNGUZI WA KAMBI YA WATOTO (ARIEL CAMP) ILIYOANDALIWA NA SHIRIKA LA AGPAHI

$
0
0
Muonekano wa Meza kuu katika ufunguzi wa kambi ya watoto (Ariel camp) wanaopata huduma katika vituo mbalimbali vya afya vinavyosaidiwa na shirika lisilo la kiserikali la AGPAHI linalofanya kazi katika mikoa ya Shinyanga na Simiyu. Ufunguzi huo ulifanyika katika hotel ya ELCT Mjini Bukoba.
Mkurugenzi wa  shirika lisilo la kiserikali la AGPAHI Bw. Laurean Bwanakunu akiongea katika ufunguzi huo uliofanyika katika hotel ya ELCT  Mjini Bukoba siku ya jana June 15,2015
 Sehemu ya watoto wakimsikiliza mgeni Mkurugenzi.
Ifuatayo ni hotuba fupi iliyotolewa na  Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la AGPAHI, Bw. Laurean Bwanakunu (aliyeko pichani)

·        Mkurugenzi Mtendaji wa AGPAHI,
·        Meneja Mradi wa AGPAHI – Shinyanga & Simiyu.,
·        Madaktari kutoka Chama cha Madaktari wa Watoto Tanzania,
·        Wafanyakazi wa AGPAHI,
·        Walezi wa watoto
·        Watoto wa Kambi ya Ariel,
·        Waandishi wa Habari,
·        Wageni Waalikwa,
·        Mabibi na Mabwana
Napenda kuushukuru uongozi wa Shirika la Ariel Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI) kwa kuandaa kambi hii ya watoto hapa Bukoba na kunikaribisha kuwa Mgeni Rasmi kwenye ufunguzi wa kambi hii.
Ninayo furaha kubwa sana kuwa nanyi hapa na kwa niaba ya Idara ya Afya ya Mkoa wa Kagera. Nawakaribisha sana mkoani kwetu!

Nimefahamishwa kwamba, shirika la AGPAHI linafanya huduma hizi za kisaikolojia kwa watoto katika mikoa ya Shinyanga na Simiyu tangu kuanzishwa kwake mwaka 2011.
Nawapongeza kwa kuendelea kuunda vikundi vidogo vidogo vya watoto katika vituo vya kutolea huduma za afya ambapo hadi sasa, mmenieleza mna jumla ya vikundi vipatavyo 35 (vyenye watoto 1,541). Nafurahi pia kusikia kuwa wilaya zote za mikoa ya Shinyanga na Simiyu zimewakilishwa katika kambi hii. Hii inaashiria kuwa AGPAHI inatambua umuhimu na thamani ya huduma za kisaikolojia kwa watoto.
Pia nimefahamishwa kuwa katika mikoa ya Shinyanga na Simiyu, kuna jumla ya watoto 694,451,kati yao watoto 6,321 wanaishi na maambukizi ya virusi vya Ukimwi.

Nimefarijika kusikia kwamba, kutokana na vikundi hivi vya huduma za kisaikolojia kwa watoto, AGPAHI ilifanya juhudi za kuanzisha kambi za watoto ambazo hufanyika mara mbili kwa mwaka. Kambi hii ya Kagera ni ya tano kufanyika chini ya uratibu wa shirika la AGPAHI. Kambi mbili za mwanzo zilifanyika mkoani Mwanza na kambi ya tatu na ya nne zilifanyika mkoani Kilimanjaro. Kambi hizi huwakutanisha watoto ili kujifunza mambo mbali mbali kuhusu afya, stadi za maisha, kupata ushauri wa kisaikolojia kutokana na changamoto wanazokutana nazo na pia huduma za kitabibu kutoka kwa madaktari bingwa wa watoto katika kipindi cha kambi. Pia, kambi hizi huwajenga vijana na kuwafanya mabalozi wa huduma za watoto katika jamii.

Vilevile, naomba kuchukua fursa hii, kuwasihi watoto mzingatie masomo, kanuni za afya kama mnavyoelekezwa na wataalam wa afya na endeleeni kuwa wanachama wazuri katika vikundi vya watoto vinavyosimamiwa na AGPAHI.

Pia, ningependa kuwashukuru walezi ambao wamesafiri na watoto kutoka mikoa ya Shinyanga na Simiyu. Napenda mpeleke shukrani kwa walezi wengine waliobaki kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kuunda vikundi vya watoto, kuwalea watoto katika maadili mazuri ya kitanzania na kuwaelimisha juu ya huduma za afya.

Mwisho ningependa kuwatakia watoto wote kambi njema. Mzingatie mafunzo na nawatakieni kila heri kwa safari ya kwenda kutembelea mto Kagera, kiwanda cha sukari Kagera, makumbusho ya vita vya Idd Amin na mpaka wa Tanzania na Uganda siku ya Jumatano.
Baada ya kusema hayo machache, sasa napenda kutamka rasmi kuwa, kambi ya Ariel 2015 mkoani Kagera imefunguliwa.
ASANTENI KWA KUNISIKILIZA!
Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa, Bw. Herman Kabirigi (Afisa Afya wa Mkoa wa Kagera) ambaye ndiye alikuwa Mgeni Rasmi katika ufunguzi wa kambi ya siku tano ya watoto (Ariel -Camp ) inayofanyika katika hotel ya ELCT  Mjini Bukoba akihutubia. 
Madaktari kutoka Chama cha Madaktari wa Watoto Tanzania - Dr. Festo Manyama na Dr. Maimuna Ahmed katika hali ya Usikivu.
Bwana Jasson Lwankomezi ambaye ni mtaalam wa Saikolojia akitoa maelezo kwa watoto hao.
Bi Cecilia Yona akitoa ufafanuzi wakati wa kuanza kambi.
 Watoto wakiwa tayari kujibu maswali .
 Zoezi la utambulisho likiendelea
 Pichani kushoto ni Dr. Scott Amos, Dr Maimuna Ahmed na Dr. Festo Manyama wakati wa utambulisho.
 Bw. Milton Kuhoyelwa ambaye ni mhudumu wa afya kutoka Maswa akisalimia washiriki.
 Muendelezo wa matukio wakati wafanyakazi wa AGPAHI na walezi wa watoto wakiwajibika
 Dr. Festo Manyama akitolea jambo ufafanuzi
Bw. Gastor Njau akizungumza.
Mr. Mugisha akiwajibika katika kupata matukio kwa ajili ya kumbukumbu.

Wafanyakazi wa AGPAHI - Bi Jane Shuma na Bw. Emilian Ng'wandu.
Muonekano wa Menu husika.
Mmoja ya watoto akipata huduma ya Chakula
Waalikwa wakiendelea kupata huduma ya Chakula katika hotel ya ELCT Bukoba .
Taswira mbalimbali wakati watoto  wakishiriki michozo.
Watoto wakiwa katika michezo.
Kwenye viwanja vya Gymkhana Mjini Bukoba watoto hao wakionyesha uwezo wao katika kucheza mpira wa miguu.
Muendelezo wa matukio mbalimbali katika picha.

IFUATAYO NI  HOTUBA FUPI YA MGENI RASMI KATIKA UFUNGUZI WA KAMBI YA WATOTO (ARIEL CAMP) ILIYOFANYIKA ELCT BUKOBA HOTEL - 15/06/2015

·        Mkurugenzi Mtendaji wa AGPAHI,
·        Meneja Mradi wa AGPAHI – Shinyanga & Simiyu.,
·        Madaktari kutoka Chama cha Madaktari wa Watoto Tanzania,
·        Wafanyakazi wa AGPAHI,
·        Walezi wa watoto
·        Watoto wa Kambi ya Ariel,
·        Waandishi wa Habari,
·        Wageni Waalikwa,
·        Mabibi na Mabwana 
Napenda kuushukuru uongozi wa Shirika la Ariel Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI) kwa kuandaa kambi hii ya watoto hapa Bukoba na kunikaribisha kuwa Mgeni Rasmi kwenye ufunguzi wa kambi hii.
Ninayo furaha kubwa sana kuwa nanyi hapa na kwa niaba ya Idara ya Afya ya Mkoa wa Kagera. Nawakaribisha sana mkoani kwetu!
Nimefahamishwa kwamba, shirika la AGPAHI linafanya huduma hizi za kisaikolojia kwa watoto katika mikoa ya Shinyanga na Simiyu tangu kuanzishwa kwake mwaka 2011.
Nawapongeza kwa kuendelea kuunda vikundi vidogo vidogo vya watoto katika vituo vya kutolea huduma za afya ambapo hadi sasa, mmenieleza mna jumla ya vikundi vipatavyo 35 (vyenye watoto 1,541). Nafurahi pia kusikia kuwa wilaya zote za mikoa ya Shinyanga na Simiyu zimewakilishwa katika kambi hii. Hii inaashiria kuwa AGPAHI inatambua umuhimu na thamani ya huduma za kisaikolojia kwa watoto.
Pia nimefahamishwa kuwa katika mikoa ya Shinyanga na Simiyu, kuna jumla ya watoto 694,451,kati yao watoto 6,321 wanaishi na maambukizi ya virusi vya Ukimwi.
Nimefarijika kusikia kwamba, kutokana na vikundi hivi vya huduma za kisaikolojia kwa watoto, AGPAHI ilifanya juhudi za kuanzisha kambi za watoto ambazo hufanyika mara mbili kwa mwaka. Kambi hii ya Kagera ni ya tano kufanyika chini ya uratibu wa shirika la AGPAHI. Kambi mbili za mwanzo zilifanyika mkoani Mwanza na kambi ya tatu na ya nne zilifanyika mkoani Kilimanjaro. Kambi hizi huwakutanisha watoto ili kujifunza mambo mbali mbali kuhusu afya, stadi za maisha, kupata ushauri wa kisaikolojia kutokana na changamoto wanazokutana nazo na pia huduma za kitabibu kutoka kwa madaktari bingwa wa watoto katika kipindi cha kambi. Pia, kambi hizi huwajenga vijana na kuwafanya mabalozi wa huduma za watoto katika jamii.
Vilevile, naomba kuchukua fursa hii, kuwasihi watoto mzingatie masomo, kanuni za afya kama mnavyoelekezwa na wataalam wa afya na endeleeni kuwa wanachama wazuri katika vikundi vya watoto vinavyosimamiwa na AGPAHI.
Pia, ningependa kuwashukuru walezi ambao wamesafiri na watoto kutoka mikoa ya Shinyanga na Simiyu. Napenda mpeleke shukrani kwa walezi wengine waliobaki kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kuunda vikundi vya watoto, kuwalea watoto katika maadili mazuri ya kitanzania na kuwaelimisha juu ya huduma za afya.
Mwisho ningependa kuwatakia watoto wote kambi njema. Mzingatie mafunzo na nawatakieni kila heri kwa safari ya kwenda kutembelea mto Kagera, kiwanda cha sukari Kagera, makumbusho ya vita vya Idd Amin na mpaka wa Tanzania na Uganda siku ya Jumatano.
Baada ya kusema hayo machache, sasa napenda kutamka rasmi kuwa, kambi ya Ariel 2015 mkoani Kagera imefunguliwa.
ASANTENI KWA KUNISIKILIZA!

 Watoto wakipata chai ya Jioni .



 







Viewing all articles
Browse latest Browse all 4177

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>