Ngoma za masikio ya mwanalibeneka wenu (kiranja)wa Bukobawadau Blog yamenasa fununu za kuwepo kwa pati ya aina yake mwishoni mwa wiki hii itakayo fanyika ndani ya Ukumbi wa Linas Night Club.
Ndipo tukaanza kuandaa ‘patroo’ maalumu ili kunasa habari za hapa na pale kujua ni nini kitakachojili na patakuwa na matukio yapi muhimu.
Chanzo chetu kinabaini kuwa, maandalizi ya sherehe hiyo tayari yameingiliwa kati kati na Mme wake Mdau Abdulrahim Mawenya (Mr Simba) na kumzuia BI Rukia asitumie fedha zake na kwamba kila kitu na gharama zote za juu zitakuwa juu yake.
Akizungumza na waandishi wetu kwa usiri na sauti ya ‘kimbeya’, mmoja wa rafiki wa Diamond (jina kapuni) aliweka wazi kwamba Mr Simba amepania kumfanyia Mke wake mpendwa pati hiyo ikiwa ni moja ya matukio yatakayoendelea kukumbukwa kwa mwaka huu.
“Bwana Abdulrahim Simba amepania kufanya makubwa kwenye sherehe hiyo ya kuzaliwa ya MKEWE ikiwa ni moja ya matukio yake muhimu yatakayokumbukwa. Itakuwa ni pati ya kufa mtu,” alisema
Katika moja ya maandalizi ya sherehe hiyo itakayo fanyika siku ya UZINDUZI WA MBIO ZA MWENGE KITAIFA MJINI HAPA tayari wamealikwa watu maalum ,pia vikundi vya burudani na wacheza show maalum.
Katika sherehe hiyo ambayo Bi Rukia anatimiza miaka kadhaa tangu aanze kuvuta hewa ya oksijeni, muziki wa ladha mbalimbali utatawala; Bongo, Sebene,Kwaito, RnB, Eningiri, omutoro,okwebuga,Enchuma aka Sindika!!na nyimbo za wasanii wengineo wa hapa Nyumbani zitasikika masikioni mwa watakao hudhuria.
FANYA UWEZAVYO MDAU ,UWE MMOJA KATI YA WENYE BAHATI YA KUHUDHURIA PARTY HII!!